TEMBELEA

www.deoamon.blogspot.com

Jumatatu, 11 Novemba 2013

VYUO VYA KATI TANZANIA VIPEWE KIPAOMBELE

Wanafunzi wa chuo cha DAR ES SALAAM CITY COLLEGE  wakijisomea  wakati wa mitihani yao ya mwisho katika chuo hicho.
   
       Wanafunzi wengi wa vyuo  vya  kati  nchini Tanzania wenye  malengo ya  kufanikiwa  katika maisha  yao  kutokana  na  elimu wanayoipata  katika vyuo hivyo, wanahitaji kupewa kipaombele  kutoka serikalini kwani vyuo  hivyo vinatoa  elimu inayowasaidia vijana wengi katika nchi  yetu.
      Vyuo hivyo  vinavyotoa elimu ya  cheti na Stashahada  vimekuwa  chachu ya  kufaulisha wanafunzi wengi wanaojiunga na elimu  ya juu  nchini. Tofauti  na elimu  ya  sekondari  inayotolewa nchini  ambayo  imeonekana kusuasua katika miaka  ya  hivi  karibuni , vyuo vya kati vimebaki kama nguzo  na msingi imara wa elimu katika nchi  yetu.
       Aidha  vyuo hivyo vimekuwa  vikivumbua  vipaji tofauti  kwa vijana tofauti katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania, baadhi  ya  fani  zanazotolwa katika vyuo  hivyo  ni Uandishi wa Habari ,Utawala, Ununuzi na Ugavi, Maendeleo ya Jamii pamoja na fani nyingine nyingi zinazoweza kuinua  na kuendeleza maendeleo ya  nchi yetu.
       Baadhi ya  vyuo  vinavyotoa  elimu  ya  cheti na  Stashahada katika  fani mbalimbali nchini  ni pamoja na  ROYAL  COLLEGE OF TANZANIA, DAR ES SALAAM CITY COLLEGE, TIMES SCHOOL OF JOURNALISM, DATASTAR  TRAINING COLLEGE  vyote   vya jijini  Dar  es salaam, ARUSHA JOURNALISM TRAINING  COLLEGE, NATIONAL COLLEGE OF TOURISM, Vya jijini Arusha.
      Imetolewa  na Deo Amon, ARUSHA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.