TEMBELEA

www.deoamon.blogspot.com

Alhamisi, 31 Oktoba 2013

MTOMTO AKUTWA AMEFARIKI NDANI YA SHIMO LA CHOO

 MBEYA,

              Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mtoto Joshua Isack (4) aliyepotea nyumbani kwao akiwa anacheza na watoto wenzie kwa siku tatu akutwa akiwa amefariki dunia ndani ya shimo la choo cha jirani na kuzua sintofahamu  kwa  majirani  na  ndugu,

       

             Mwili wa Mtoto Joshua Isack (4) ukichukuliwa na polisi

                  Hili ndilo shimo alimokutwa  marehemu Joshua

 Tukio hilo la kuonekana kwa mtoto huyo lilitokea jana majira ya saa Kumi jioni katika Mtaa wa Nyibuko Pambogo kata ya Iyela Jijini Mbeya baada ya juhudi za wazazi na majirani kushirikiana kumtafuta na kumpata akiwa amepoteza maisha ndani ya shimo la choo. 

         Akizungumza kwa uchungu na masikitiko makubwa baba mzazi wa marehemu Isack Daniel ambaye ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Maji Mbeya alisema Mtoto wake huyo wa kiume alikuwa anacheza na wenzie jumatatu ya Oktoba 28,  majira ya saa 12 jioni lakini alitoweka katika mazingira ya kutatanisha. 

          Alisema baada ya kuona giza linaingia na mtoto hajarudi alianza kumtafuta katika kila eneo akishirikiana na baadhi ya ndugu na majirani lakini hakufanikiwa kumwona kwa siku hiyo ambayo kesho yake akiwa ni viongozi wa mtaa walienda kutoa taarifa kituo cha Polisi cha Kati Mbeya Mjini. 

          Mzazi huyo aliendelea kusema baada ya kutoa taarifa polisi bado waliendelea na juhudi za kumtafuta huku Ubalozi ukiunda kikosi maalumu cha kufanya msako wa nyumba hadi nyumba ambapo baada ya kupita katika nyumba ya jirani alipokutwa marehemu katika shimo la maji machafu walipatwa na wasi wasi baada ya kuona kuna mabadiliko ya mbao zilizokuwa zimefunika shimo hilo. 

          Alisema awali walivyopita siku moja kabla waliona shimo hilo likiwa limefunikwa kwa mabanzi yaliyochakaa lakini siku ya pili yake asubuhi walikuta kukiwa na mabanzi mapya kuashiria kuna ukarabati umefanyika hali iliyowapa wasi wasi na kulazimika kulifunua shimo hilo na kumkuta marehemu akiwa amepoteza maisha ndani ya shimo  hilo.,

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.