Mbeya.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amemmwagia sifa Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana akisema amefanya kazi nzuri kwa kuwafikisha mawaziri wanne kwenye Kamati Kuu baada ya kubaini matatizo yanayohusu sekta zao.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amemmwagia sifa Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana akisema amefanya kazi nzuri kwa kuwafikisha mawaziri wanne kwenye Kamati Kuu baada ya kubaini matatizo yanayohusu sekta zao.
Rais
Kikwete alisema jana kuwa katika ziara ya viongozi wa Sekretarieti ya
CCM mwishoni mwa mwaka jana, kwenye mikoa ya Ruvuma na Mbeya, Kinana
alifanya kazi nzuri katika mazingira magumu kiasi cha kufikia kupanda
meli kwenye Ziwa Nyasa.
Alisema akiwa kwenye ziara
hiyo, Katibu Mkuu huyo aligundua matatizo kadhaa kwenye sekta za
mawaziri husika na hivyo aliamua kuwafikisha Kamati Kuu ili watoe
maelezo, jambo ambalo alisema linatakiwa kuigwa na viongozi wengine wa
CCM.
“Najua wapo watu walitaka mawaziri hao wafukuzwe
kazi. Kwa vile hilo halikufanyika, basi likageuzwa kuwa suala la
malumbano. Napenda ieleweke kuwa kuitwa Kamati Kuu hakuna maana ya
kuishia kufukuzwa,’’ alisema Kikwete. Alisema mawaziri hao waliitwa kwa
sababu matatizo yaliyobainika yalitakiwa kupatiwa ufumbuzi na kwamba
yalitolewa maelekezo kwa ajili ya utekelezaji.
Alisema
Kamati Kuu inaendelea kufuatilia na kama hakutakuwa na maendeleo ndipo
inapoweza kuomba mamlaka ya uteuzi ichukue hatua zinazotakiwa dhidi ya
wahusika.
“Hongera Ndugu Kinana kwa kusimamia na kutekeleza kwa vitendo maazimio ya Mkutano Mkuu wa chama chetu,” alisema Kinana.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.